Wizara ya fedha ya Marekani imetangaza vikwazo vipya dhidi ya watu binafsi saba na mashirika matatu ya Korea Kaskazini kutokana na kuhusika na ilichodai kuwa ni ukiukaji wa haki za binadamu. Watu binafsi waliowekewa vikwazo hivyo ni pamoja na maofisa wa usalama wa jeshi la Korea Kaskazini, waziri wa leba Jong Yong Su, konsela mkuu wa nchi hiyo mjini Shenyang, China na mwanadiplomasia mwingine katika ubalozi wake nchini Vietnam.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |