Kiungo wa Manchester City, Yaya Toure anajiandaa kutua katika klabu ya New York City FC ya Marekani ambayo ni klabu dada ya Manchester City, wakati huu akionekana kama mbadala halisi wa kiungo mkongwe, Andrea Pirlo anayeelekea kustaafu.
Toure hana nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha kocha, Pep Guardiola na aliongezewa mkataba wa mwaka mmoja tu mwishoni mwa msimu uliopita, lakini hatazamiwi kuongezewa mkataba mwingine mwishoni mwa msimu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |