Wizara ya Ulinzi ya Afghanistan imetangaza kuwa jumla ya wapiganaji 95 wameuawa kwenye operesheni mpya ya kijeshi nchini humo.
Jeshi la Ulinzi wa Taifa na Vikosi vya Usalama ANDSF vilianzisha operesheni ya kusafisha baadhi ya maeneo yenye magaidi na maadui wanaovuruga amani na utulivu wa nchi hiyo kwa saa 24. Na matokeo yake, magaidi 95 waliuawa, wanane kujeruhiwa na 11 walikamatwa na vikosi vya usalama. Vikosi hivyo pia vimekamata silaha na risasi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |