Serikali ya Uingereza imetoa tahadhari ya usafiri kwa raia wake wanaopang kusafiri nchini Kenya kwa shughuli za kitalii.Uingereza imewataka raia wake kutoelekea maeneo ya magharibi mwa Kenya ikisema kuna uwezekano wa ghasia kutokea katika maeneo hayo.Taarifa hiyo inakuja wakati ambapo idadi ya watalii wanaozuru Kenya ikiendelea kupungua na kuwa pigo kwa sekta ya utalii nchini Kenya. Aidha Uingereza imewataka raia wake walioko Kenya kutazama vyombo vya habari ili kujua ni sehemu zipi ambazo ni hatari kwa watalii.Mwezi jana, Kenya ilipunguza makadirio yake ya ukuaji wa uchumi hadi asilimia 5.5 kutokana na kile ilichotaja kuwa ukame na msukosuko wa kisiasa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |