Jeshi la muungano unaoongozwa na Saudi Arabia limefanya mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje na wanadhimu wakuu wa majeshi, ili kuratibu operesheni za kijeshi, kidiplomasia na kibinadamu nchini Yemen. Mnadhimu mkuu wa jeshi la Saudi Arabia Abdul Rahman amesema lengo la muungano huo ni kuhakikisha serikali halali ya Yemen inaweza kutekeleza madaraka yake kote nchini Yemen. Ripoti iliyotolewa na Umoja wa mataifa inasema zaidi ya raia elfu tano, wakiwemo watoto elfu moja, wameuawa tangu mgogoro wa Yemen ulipuke.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |