Serikali ya jimbo la Oromia la Ethiopia imetangaza kuwakamata watu 245 wanaotuhumiwa kufanya ghasia katika jimbo hilo.
Msemaji wa serikali ya jimbo hilo Bw Addisu Arega amesema, maandamano ya kimabavu yaliyotokea hivi karibuni yamesababisha vifo vya watu 11, gari moja kuchomwa na kuhujumu shughuli za kiuchumi za kawaida. Amesema watu kadhaa wamekamatwa kuhusiana na maandamano hayo na pia wanatuhumiwa kuchochea chuki kati ya makabila tofauti.
Hali kwa sasa imedhibitiwa kutokana na juhudi za serikali kuu na serikali ya jimbo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |