Mnadhimu mkuu wa jeshi la Iran Mohammad Bagheri amesema, kama Marekani itaiwekea Iran vikwazo vipya, Iran itajitoa kwenye makubaliano ya nyuklia.
Bw. Bagheri amesema nia ya Iran kusaini makubaliano hayo ilikuwa ni kuondoa vikwazo ilivyowekewa na nchi za magharibi, na kwamba kama Iran itawekewa upya vikwazo, makubaliano hayo hayatakuwa na maana yoyote.
Rais Donald Trump wa Marekani tarehe 13 mwezi huu alikataa kutambua kuwa Iran inatekeleza makubaliano, na alitangaza kuwa Marekani itaweka vikwazo dhidi ya kikosi cha mapinduzi cha Kiisalmu cha Iran.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |