Waziri wa mambo ya nje wa Russia Bw. Sergei Lavrov amesema shutuma kuwa Russia iliingilia uchaguzi mkuu wa Marekani au wa Umoja wa Ulaya, hazina msingi wowote, na watungaji wa shutuma hizo hawawezi kutoa ushahidi wowote. Bw. Lavrov amesema uchunguzi kuhusu uingiliaji wa Russia kwenye uchaguzi mkuu wa Marekani umeendelea kwa miezi tisa, lakini hakuna ushahidi wowote uliotolewa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |