• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Baraza la usalama la UN lasisitiza kulinda haki na maslahi ya watoto kwenye migogoro ya kijeshi

    (GMT+08:00) 2017-11-01 09:37:10

    Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limetoa taarifa likisisitiza umuhimu wa kulinda haki na maslahi ya watoto kwenye migogoro ya kijeshi.

    Taarifa hiyo inazihimiza pande mbalimbali za migogoro ziheshimu kazi ya mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa na washirika wao, na kuwaruhusu watoe misaada kwa watoto kwa usalama, kwa wakati na bila vizuizi.

    Taarifa inasema Baraza la usalama linalaani vitendo vya kuwatumikisha watoto jeshini, kuua, kubaka na kuteka nyara watoto, na kushambulia shule na hospitali, na kuzitaka pande zote zinazopambana zisitishe mara moja vitendo hivyo na kuchukua hatua maalum kulinda usalama wa watoto.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako