• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Maafisa wa uvuvi wahimizwa kuongeza bidii

    (GMT+08:00) 2017-11-02 20:28:50

    Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amewataka maofisa wa forodha wa Sirari wilayani Tarime kuongeza juhudi katika kulinda rasirimali ili kuunga mkono kasi ya Rais Dk John Mafuguli ya kulinda rasirimali hizo.

    Ulega alieleza hayo wakati akizungumza na wafanyanyakazi wa forodha hiyo katika kikao kati yake na watendaji baada ya kufanya ziara katika eneo hilo.

    Naibu Waziri huyo alitoa kauli hiyo, baada ya kuelezwa kwamba wilaya hiyo haina tatizo la mifugo kutoka nje ya nchi na kuingia nchini lakini kumekuwa na tabia kwa baadhi ya madalali kutorosha mifugo na kuuza nchi jirani ya Kenya.

    Aliwaataka watendaji hao kutobabaika bdala yake wasimamie sheria na kufanya kazi kwa uadilifu ikiwamo kushirikiana ili kudhibiti hali hiyo inarudisha nyuma jitihada za Serikali za kuleta maendeleo

    Pia Ulega alitumia nafasi kuwaeleza watumishi hao kwamba wizara itahakikisha kituo cha ukaguzi wa mifugo cha Kirumi wilayani Butiama kinafanya kazi kwa ufanisi kuwa kuweka miundombinu ya maji na umeme ili mnada uliopo uanze kufanya kazi.

    Kabla ya kwenda katika forodha hiyo, Ulega alipat fursa ya kuonana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima na walipeana mikakati mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha sekta ya mifugo na uvuvi inasonga mbele

    Katika mazungumzo yao viongozi hao walikubaliana suala La kudhibiti uvuvi haramu Hasa unaofanyika katika ziwa Victoria ambapo Malima alimwahidi Ulega kwamba atahakikisha anatumia vyombo Vya Dola ILI kukabiliana Na Hali.

    Wakati Malima akieleza Hayo, Ulega Naye alimwakikishia kwamba wizara hiyo itakuswa Bega Kwa Bega kushirikiana Na mkoa huo katika kuhakikisha sekta hizo zinapiga hatua na kusonga mbele

    Mbali na hilo, viongozi hao walikubaliana kuanza kwa mchakato wa kufufua viwanda vya kusindika samaki na nyama vilivyopo ili kuunga mkono jitihada za Dk Magufuli za Tanzania ya viwanda ili kuwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako