Jeshi la Syria limetwaa udhibiti wa eneo muhimu kwa kundi la Islamic State mjini Deir al-Zour, mashariki mwa nchi hiyo, baada ya kupambana na kundi hilo. Chanzo cha habari kinasema jeshi hilo na wapiganaji washirika wametwaa eneo la Hamidiyeh lenye vituo vingi vya uongozi wa kundi la IS, na kwamba hivi sasa bado kuna maeneo yanayodhibitiwa na kundi hilo mjini Deir al-Zour, akikanusha ripoti inayodai kuwa jeshi la Syria limetwaa udhibiti kamili wa mji huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |