Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wilfred Kidau amesema tayari Tanzania imethibitisha kushiriki mashindano ya Challenge yatakayoanza Novemba 25 hadi Desemba 9 nchini Kenya, huku yakipangua ratiba ya Ligi Kuu Bara. Kidau alisema awali hawakuyaweka kwenye ratiba mashindano hayo kwa sabababu hawakuwa na uhakika kama yatafanyanyika. Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura alisema timu za Taifa zinapokuwa kwenye mashindano lazima ratiba ibadilike hivyo watafanya mabadiliko ya ratiba ya ligi lakini watahakikisha haiathiri fainali ya Kombe la Shirikisho (FA).
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |