Nchini Libya, Naibu Waziri wa mambo ya ndani wa serikali ya umoja, Faraj Aqim amenusurika kifo baada ya msafara wake kushambuliwa na mlipuko wa bomu lililokuwa limetegwa katika gari lililoegeshwa kando ya barabara mjini Benghazi.
Akizungumza na televisheni ya Libya, Bw Aqim amethibitisha kuwa shambulizi hilo halikumdhuru, isipokuwa limewajeruhi walinzi wake.
Licha ya kwamba Serikali imelitaja tukio hilo kuwa ni dhaifu, taarifa zinasema hali bado si shwari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |