Marekani imekubali kuanza kutoa viza katika ubalozi wake mjini Ankara nchini Uturuki, ikiwa ni mwezi mmoja tangu isitishe mpango huo kufuatia mvutano uliojitokeza baina ya mataifa hayo mawili.
Katika taarifa iliyotolewa jana, Ubalozi wa Marekani umesema umehakikishiwa na serikali ya Uturuki kwamba watu hakuna maofisa wa ubalozi wa Marekani ambao wanachunguzwa, na kwamba itaiarifu Marekani kama kuna ofisa inayetaka kumkamata au kumweka kizuizini. Hatua hii imefikiwa kufuatia ziara ya siku nne ya waziri mkuu wa Uturuki Bw. Binali Yildirim nchini Marekani, ambaye pia anatarajiwa kufanya mkutano na makamu wa Rais wa Marekani Bw. Mike Pence.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |