Wizara ya kilimo nchini Kenya imefuta uagiziaji wa magunia 550,000 ya mahindi na 20,000 ya mchele.
Awali halmashauri ya nafaka nchini humo ilikuwa imeweka tangazo la kuagiza kutoka nje bidhaa hizo.
Mkurungezi wa halmashauri hiyo Newton Terer amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya kushauriana na wizara ya kilimo.
Terer pia amesema halmashauri hiyo ndio pekee itakayoshughulikia uagiziaji wa nafaka iwapo utahitajika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |