Rais wa Rwanda Paul Kagame amepewa tuzo kwa juhudi zake za kukuza utalii endelevu na utunzaji wa mazingira.
Tuzo hilo limetolewa na waandalizi wa maonyesho ya World Travel Market, ambayo yanaendelea mjini London, Uingereza.
Waandalizi walisema rais Kagame amechukua hatua za kuwekeza katika miundo mbinu na kuifanya Rwanda kuwa kituo muhimu cha utalii na uwekezaji.
Akizungumza kwenye hafla ya kupokea tuzo hilo Kagame amsema Rwanda iko kwenye hatua za kuongeza safari zake za ndege kufikia maeneo mengi zaidi duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |