Msemaji wa bunge la Libya Bw Abdullah Bilhag, amesema bunge hilo limeiagiza kamati ya maridhiano kuwasiliana na jeshi na serikali ya mpito ili kusitisha mara moja mapigano yanayoendelea katika eneo la Warshaffana, magharibi mwa nchi hiyo.
Bw Bilhag amesema bunge hilo limeazimia kufuatilia kwa karibu taarifa za watu wanaosakwa mjini Warshaffana, kwa kutumia njia madhubuti kupitia vikosi vya usalama vyenye weledi na majeshi ya Libya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |