Chama cha wanaviwanda na wafanyabiashara wa Namibia (NCCI) kimesaini makubaliano na Baraza la Maendeleo ya Biashara za Kimataifa la China (CCPIT). yatakayohimiza mashirikiano ya kibiashara na kiuwekezaji baina ya mataifa hayo mawili.
Akizungumza wakati wa kusaini makubaliano hayo mkurugenzi wa NCCI Bibi Esther Akwaake amesema Namibia inatarajia kunufaika na maendeleo ya China.
Maeneo makubwa ambayo washirika wawili hao wataangazia ni kilimo, miundo mbinu na sekta ya nishati endelevu.
.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |