• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Langalanga: Hamilton asema jinamizi la kodi halimuathiri kubeba taji

    (GMT+08:00) 2017-11-09 08:43:37

    Lewis Hamilton amesema hataruhusu mzozo unaomkabili wa kuchunguzwa kwa kutolipa kodi kumuathiri wakati ambao anaelekea kumaliza mbio mbili za mwisho kwenye mashindano ya magari msimu huu. Dereva huyo wa Mercedes, alikiri jana huko Sao Paulo kuwa kwa sasa kuna jinamizi linalomwandama lakini atahakikisha baada ya mashindano anaondoka na taji la Brazil Grand Prix. Hamilton ambaye amejinyakulia taji lake la nne la dunia katika mbio za mwisho za Mexico, amedhamiria kushinda mbio za Jumapili huko Interlagos na zile za Novemba 26 zitakazofanyika Abu Dhabi. Mkimbiza gari huyo ni miongoni mwa nyota maarufu ambao wameingia kwenye uchunguzi wa kodi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako