Bodi ya ligi nchini Tanzania TPLB imetoa onyo kali kwa klabu ya Simba pamoja na kuipiga faini baada ya kubaini makosa kadhaa ambayo yalifanywa na klabu hiyo kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Njombe Mji. Mkurugenzi mtendaji wa bodi hiyo Boniface Wambura amesema Simba imeonywa kwa kosa la kumsimamisha kwenye benchi la ufundi kocha wao msaidizi Masoud Juma raia wa Rwanda kwenye mchezo wao na Njombe Mji bila kuwa na vibali vya kufanya kazi nchini. Mbali na onyo hilo klabu ya Simba imeadhibiwa kwa kupigwa faini ya Tsh. 300,000 kwa kosa la kuchelewesha kuwasilisha orodha ya majina ya wachezaji waliocheza mchezo wa siku hiyo. Aidha
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |