Jeshi la Uganda limesema litawaondoa askari wake wa kulinda usalama nchini Somalia hatua kwa hatua kuanzia mwishoni mwa mwezi ujao, kwa kufuata uamuzi wa Umoja wa Afrika na baraza la usalama la Umoja wa Mataifa.
Msemaji wa jeshi la Uganda Brigedia Richard Karemire amesema Uganda imeandaa mpango wa kuwaondoa askari zaidi ya 6000 wanaotoa huduma katika tume ya Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM kabla ya tarehe 31 Desemba.
Msemaji huyo ameongeza kuwa mpango huo umeandaliwa baada ya vikosi vya kulinda usalama vya Somalia kupata uwezo wa kulinda usalama wa nchi hiyo
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |