Umoja wa Ulaya umefuta zuio la Ghana la kuuza mbogamboga katika mataifa ya Ulaya baada ya kujiridhisha kwamba kwa sasa bidhaa hizo zimekidhi vigezo vya usalama. Miaka mitatu iliyopita Umoja wa Ulaya uliwazuia wafanyabiashara wa Ghana kuuza bidhaa zao barani Ulaya kwa kile kilichodaiwa kuwa ni ubora hafifu na kutokuwa na vifungashio salama. Inakadiriwa kuwa Ghana imepoteza takribani dola za kimarekani milioni 30 baada ya kuzuiwa kusafirisha mboga mboga kwenda katika soko la ulaya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |