• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Umoja wa mawasiliano ya simu wa Afrika watoa wito wa kuboresha maisha ya watu kupitia internet

    (GMT+08:00) 2017-11-09 19:04:31
    Katibu mkuu wa Umoja wa Mawasiliano ya Simu wa Afrika ATU Bw. Abdoulkarim Soumaila amesema ni muhimu kuvifanya vijiji na sehemu za pembezoni barani humo vipate fursa za kiuchumi kupitia internet.

    Bw. Soumaila amesema hayo kwenye mkutano wa baraza la teknolojia ya habari na mawasiliano la Afrika, uliofanyika wakati wa maonyesho ya Mawasiliano ya Simu ya Afrika nchini Afrika Kusini. Amesema kuungana na internet kunaweza kubadilisha maisha ya watu katika sekta nyingi, ikiwemo afya, elimu, huduma za kifedha, kilimo, na kadhalika.

    Kwa upande wake, mkuu wa kampuni ya Huawei eneo la Kusini mwa Afrika, Bw. Li Peng amesema watunga sera wa nchi nyingi za Afrika wameweka mazingira mazuri kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya teknolojia ya habari na mawasiliano, na kwamba makampuni yamefanya kazi muhimu katika kutoa teknolojia, ufumbuzi, huduma na mafunzo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako