• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Manchester United yatandwa na hofu juu ya kocha wake Jose Mourinho

    (GMT+08:00) 2017-11-10 09:15:19

    Klabu ya Manchester United imenza kuwa na hofu juu ya kocha Jose Mourinho kwani anahisiwa kuikimbia ligi ya Epl kutokana na ushindani mkubwa. Pep Gurdiola anatajwa kama sababu ya kumkimbiza Jose Mourinho kwani inaonekana Mourinho anaamini kwa sasa hawezi kushindana na Pep Gurdiola anayeonekana kuwa tishio kubwa hivi sasa.

    Jose Mourinho anahusishwa na kutua katika klabu ya PSG tetesi ambazo zilishawahi kuibuka mara ya kwanza lakini baadae zikazima lakini hivi sasa inasemekana kuna ukweli kuhusiana na jambo hilo. Mourinho ndio kwanza yuko nusu ya mkataba wake ambapo aliahidi msimu huu anaweza kufanya makubwa, japo hadi sasa hawako katika nafasi mbaya lakini tayari ameshawahi kuongelea kutamani kwenda Ufaransa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako