Rais Xi Jinping wa China amesema China na Marekani zinatakiwa kuwa wenzi badala ya wapinzani, na zikishirikana wzitanufaishana na kuinufaisha dunia nzima.
Rais Xi Jinping amesema hayo kwenye tafrija ya kumkaribisha rais Donald Trump wa Marekani katika jumba la mikutano la umma. Pia amesema anaamini kuwa changamoto za uhusiano kati ya nchi mbili zina ukomo, lakini fursa za maendeleo ya uhusiano huo hazina ukomo. Rais Trump amekubaliana na maoni hayo.
Rais Xi amesema nchi mbili zikishikilia kuendeleza uhusiano kati yao, uhusiano huo utaweza kufungua ukurasa mpya, na kutoa mchango mpya kwa mustakabali wa binadamu wote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |