Watu 14 wamefariki dunia baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kupinduka kwenye mto Krishna katika jimbo la Andhra Pradesh nchini India. Polisi wa huko wamesema boti hiyo iliyokuwa na abiria 30 ilipinduka usiku wa Jumapili na miili ya wahanga 14 imepatikana, na kwamba kazi za uokoaji zinaendelea na uchunguzi umeanza ili kujua chanzo cha ajali hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |