Katika mashindano hayo nyota mwingereza Lewis Hamilton wa Mercedes alifanikiwa kuongoza katika mizunguko kumi ya kwanza kabla ya kuadhibiwa alipokiuka moja ya kanuni za barabara ya mashindano jambo lililomfanya aishie nafasi ya nne, huku nafasi ya pili ikienda kwa Valtteri Botas wa timu ya Mercedes na Kimi Raikonnen wa Ferari akishika nafasi ya tatu.
Huu ni ushindi wa tano kwa Vettel kwa mwaka huu pekee baada ya kushinda pia kwenye mbio za Australia, Bahrain, Ufaransa na Hungary.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |