Watu wasiopungua 34 wamefariki na wengine zaidi ya 26 kujeruhiwa baada ya treni moja yenye mabehewa 13 kuanguka kusini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Gavana wa jimbo la Lualaba Bw. Richard Muyej Mangez amesema, idadi ya vifo na majeruhi huenda ikaongezeka kutokana na mabehewa mengine yanayoendelea kuwaka moto.
Treni hiyo ilikuwa ikitokea mji wa kusini mashariki wa Lubumbashi kuelekea mji wa kusini wa Luena.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |