Gharama ya interneti nchini Uganda imeshuka kwa asilimia 73 hadi dola 70 kwa kila Mbps katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, hii tayari imedhihirisha kupungua kwa gharama za kufanya biashara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Mawasiliano ya Uganda, Godfrey Mutabazi amesema, kushuka kwa gharama imetokana na utekelezaji wa utawala wa leseni ya kizazi cha nne ambayo hivi karibuni ulipata tuzo ya tume kutoka Muungano wa Kimataifa wa Mawasiliano ( ITU).
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |