Waziri wa utalii wa Kenya, Najib Balala atakwea mlima Kenya ambao ni mlima mrefu zaidi nchini humo katika hatua za kupigia debe utalii.
Balala tayari amekwenda kwenye eneo la mlima huo kujiunga na wana mazingira, wakweaji na waandishi wa habari kushiriki shughuli hiyo ya siku tano.
Upandaji huo wa mlima Kenya pia ni sehemu ya kampeni ya kukwea milima saba ndani ya wiki 7 kote barani Afrika,
Hivi karibuni waziri Balala alichaguliwa kuwa mwenye kiti wa tume ya Umoja wa Mataifa ya Utalii barani Afrika (UNWTO) ambapo aliahidi kukuza zaidi sekta hiyo akitilia mkazo usalama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |