Msemaji wa idara ya tamwimu ya taifa ya China Bi. Liu Aihua leo hapa Beijing amesema, katika mwezi Oktoba, uchumi wa China uliendelea kwa utulivu, na marekebisho ya miundo ya uchumi yanafanywa kwa kina.
Bi. Liu Aihua amesema, ingawa baadhi ya takwimu zinashuka, lakini kwa ujumla uchumi unaendelezwa vizuri, kama unavyonekana katika pande nne, ikiwemo mahitaji ya uzalishaji ni matulivu, ukosefu wa ajira unapungua na kuwa chini ya asilimia 5, kiwango cha bei ya bidhaa kinatulia, na sifa na ufanisi wa uendeshaji wa uchumi unainuka kwa madhubuti.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |