Jeshi la Misri limewaua magaidi watatu kwenye mkoa wa Sinai kaskazini nchini humo. Msemaji wa jeshi hilo Tamer al Rifaay amesema vikosi vya jeshi hilo vimeshambulia maficho ya magaidi mkoani humo, na kuwaua magaidi watatu na kuwakamata wengine 74 wanaotuhumiwa kuunga mkono ugaidi. Mpaka sasa mashambuzi ya kigaidi yamesababisha vifo vya mamia ya polisi na askari nchini humo tangu jeshi la Misri kumwondoa madarakani aliyekuwa rais wa nchi Mohamed Morsi Julai mwaka 2013.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |