• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • WADA wapendekeza Urusi ifungiwe kushiriki Olimpiki

    (GMT+08:00) 2017-11-17 10:07:37
    Wakala wa Kimataifa wa Kuzuzia dawa za kuongeza nguvu michezoni (WADA), umependekeza kuwa Timu za Urusi zisiruhusiwe kushiriki kwenye mashindano ya Olimpiki ya majira ya baridi mwakani nchini Korea Kusini.

    Akitoa sababu za pendekezo hilo Rais wa WADA Craig Reedie, amesema taifa hilo limekuwa likifanya udanganyifu katika vipimo vya wachezaji wake na limekaidi kuwapeleka wachezaji hao nje kwa ajili ya vipimo.

    Ni mara ya pili WADA kupendekeza hivyo, baada ya kufanya hivyo pia mwaka jana wakati wa Olimpiki nchini Brazili licha ya kuwa pendekezo hilo lilitupiliwa mbali na Kamati ya kimataifa ya Olimpiki IOC.

    IOC wanafanya mkutano mkuu Disemba 5, matarajio ikiwa ni kwamba huenda wakatolea majibu pendekezo hilo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako