• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • FIFA yatangaza mfumo wa upangaji makundi kombe la Dunia 2018

    (GMT+08:00) 2017-11-17 10:25:38

    Shirikisho la mpira wa miguu duniani (FIFA) limetangaza rasmi mfumo utakaoutumika kupanga makundi 8 ya timu zitakazoshiriki mashindano ya kombe la dunia hapo mwakani nchini Urusi.

    Tangazo hili limekuja muda mfupi baada ya timu ya taifa ya Peru kukamilisha jumla ya timu 32 zilizofuzu kushiriki michuano hiyo kwa kuifunga 2-0 New Zealand katika mechi yao ya pili ya mtoano iliyofanyika mjini Lima.

    Droo ya upangaji makundi inatarajiwa kufanyika rasmi Disemba mosi mwaka huu mjini Moscow, ambapo timu shiriki awali zitaingia kwenye upangaji kwa kutatajwa kulingana na viwango vya ubora.

    Mpaka sasa, Urusi ndiyo timu pekee iliyopangwa katika kundi na iko kundi A kwa kuwa mwenyeji wa mashindano.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako