Taarifa iliyotolewa na Umoja wa Afrika inasema, mwenyekiti wa kamati ya umoja wa Afrika Bw Moussa Mahamat amesikitishwa na kupigwa mnada kwa wakimbizi wa Afrika nchini Libya kama watumwa.
Bw. Moussa Faki amelaani kitendo hicho ambacho ni kinyume na malengo ya waanzishaji wa umoja huo, na vyombo husika vya Afrika na kimataifa, ikiwemo mkataba wa haki za binadamu na kiraia wa Afrika.
Mwenyekiti huyo ametaka kusimamishwa mara moja kwa vitendo hivyo na vitendo vingine vya biashara haramu ya binadamu. Pia amekaribisha serikali ya Libya kutangaza kuchunguza uhalifu huo, na kutarajia matokeo ya kuaminika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |