Mahakama kuu ya Kenya leo imethibitisha kuwa matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika upya tarehe 26 mwezi uliopita, ni halali.
Kenya ilifanya marudio ya uchaguzi wa urais tarehe 26 mwezi Oktoba, na matokeo ya uchaguzi huo yalimpa rais Kenyatta ushindi kwa kupata asilimia 98.3 ya kura.
Kiongozi wa muungano wa upinzani wa NASA nchini Kenya Bw. Raila Amolo Odinga tarehe 31 mwezi Oktoba alisema, hatakubali matokeo ya uchaguzi huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |