Katika Kundi E, Liverpool ya Uingereza itakuwa ugenini kucheza na Sevilla, zote zikiwa katika nafasi mbili za juu, huku Spartak Moscow ya Urusi ikicheza na NK Maribor ya Slovenia.
Kundi F ni Manchester City dhidi ya Feyenoord ya Uholanzi, na Napoli watacheza na Shakthar Donetsk ya Ukraine.
Na kundi katika kundi G, Besktas ya Uturuki itapambana na mabingwa wa mwaka 2004 FC Porto ya Ureno, na Monaco itakuwa na kibarua dhidi ya RB Leipzig ya Ujerumani.
Apoel Nicossia watakuwa na kibarua kizito nyumbani nchini Cyprus kucheza na bingwa mtetezi wa michuano hiyo Real Madrid, na Borussia Dortmund itaikaribisha Tottenham ya Uingereza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |