China imempongeza Uhuru Kenyatta kwa kuchaguliwa tena kuwa rais wa Kenya baada ya Mahakama ya Juu nchini Kenya kuthibitisha ushindi wake katika marudio ya uchaguzi wa rais uliofanyika mwezi uliopita.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Lu Kang amesema, China inafurahi kuona mgogoro wa uchaguzi wa urais nchini Kenya unatatuliwa ndani ya mfumo wa kisheria. Amesema kuwa anatumai Kenya itadumisha amani na utulivu na kupata mafanikio makubwa katika maendeleo ya nchi hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |