Sera ya utafiti wa kilimo imezinduliwa mjini Addis Ababa Ethiopia ikilenga kutathmini kilimo biashara na athari zake za kiuchumi kwa wanawake, kupunguza umaskini na kujitosheleza kwa chakula barani Afrika.
Sera hiyo ya miaka 5 imeziduliwa wakati wa mkutano wa kujadili sera ya ardhi barani Afrika iliofanyika mjini humo.
Itafadhiliwa na idara ya maendeleo ya kimataifa ya uingereza Dfid na mwenyekiti wake ni Janet Edeme
Nchi nyingi barani Afrika hutegemea kilimo kwa uchumi wao lakini wakulima wengi hukosa ufadhili kujiendeleza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |