Viongozi kutoka wilaya 14 karibu na ziwa Kyoga nchini Uganda wameitaka serikali kushughulikia viwanda kadhaa vya samaki kwenye eneo hilo ambazo hazijakamilishwa kwa muda.
Wamesema wakandarasi waliopewa kazi za ujenzi bado hawajatekeleza na hivyo kuharibu raslimali.
Mradi huo ulikuwa umefadiliwa na benki ya dunia pamoja na benki ya ustawi ya Afrika.
Naye waziri wa kilimo Vincent Ssempijja amesema serikali inafanya kila iwezalo kulinda ziwa hilo dhidi ya uharibifu unaotokana na uchafuzi wa mbinu duni za uvuvi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |