Magoli hayo yaliyofungwa na Roberto Firmino mawili na Sadio Mane moja, yalidumu kipindi cha kwanza tu kabla ya Sevilla kusawazisha yote katika dakika za 51, 60 na 93 kupitia Wissam Yedder mawili na Guido Pizzaro.
Kufuatia matokeo hao, timu hizo ambazo ziko kundi E la michuano hiyo, zitasubiri hadi mechi ya mwisho ya makundi ili kujihakikishia kufuzu hatua ya 16 bora, kwa kuwa Liverpool ni vinara kwa pointi 9, Sevilla 8 na Spartak Moscow wako nafasi ya tatu wakiwa na alama 6 ambazo endapo wakishinda mechi ya mwisho dhidi ya Liverpool wanaweza kufuzu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |