Besiktas imefikisha pointi 11 na ni vinara wa kundi G, ikiwa imeshinda mechi 3, na kutoa sare mbili, lakini FC porto na RB Leipzig watalazimika kusubiri mechi za mwisho ili kujihakikishia nafasi moja iliyosalia katika kundi hilo.
Timu zingine zilizofuzu jana kuingia hatua ya kumi na sita bora ni Real Madrid ya Hispania na Tottenham Hotspurs ya Uingereza.
Madrid imefuzu kwa kuwa mshindi wa pili wa kundi baada ya kuifunga Apoel Nicossia ya Cyprus kwa magoli 6-0, na Tottenham wakiibuka vinara wa kundi hilo kwa kufikisha pointi 13 baada ya kuifunga 2-1 Borussia Dortmund jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |