• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Hatarini kukosa kombe la dunia 2018 licha ya kufuzu

    (GMT+08:00) 2017-11-24 09:41:02
    Kwa mujibu wa kanuni za FIFA, timu ya taifa ya Peru huenda ikakosa kushiriki mashindano ya kombe la dunia mwaka 2018, licha ya kwamba timu hiyo imefuzu kushiriki.

    Uamuzi huo waweza kuchukuliwa endapo serikali itapitisha muswada uliopelekwa bungeni wa kuitaka serikali iingilie masuala ya soka nchini humo.

    FIFA sasa watalazimika kutafuta timu mbadala iwapo Peru watafutwa.

    Lakini gazeti la Libero la nchini Peru limemnuku mbunge ambaye amahusika kupeleka muswada huo Paloma Noceda akiwatoa wasiwasi wananchi wa Peru kuwa hata sheria ipitishwe timu itashiriki kombe la dunia.

    Peru hawajashiriki kombe la dunia tangu mwaka 1982, na awamu hii wamefuzu baada ya kuwafunga New Zealand kwenye mechi ya mtoano.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako