CTI imesema wanashindwa kuiondoa sukari hiyo baada ya kukosa kibali cha kufanya hivyo kutoka Bodi ya Sukari kwa kile kinachoelezwa kuwa ni agizo la Serikali kuzuia uagizaji wa bidhaa hiyo.
Hata hivyo, mtaalamu wa sera wa CTI, Akida Mnyenyelwa alisema agizo hilo halikulenga sukari hiyo inayotumika viwandani kuzalisha bidhaa za aina tofauti kama vile dawa na vinywaji baridi.
Alisema kutokana na zuio hilo, baadhi ya viwanda vimekosa sukari kwa ajili ya uzalishaji wa bidhaa licha ya taratibu zote muhimu za kuingiza mzigo huo kufuatwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |