• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Sukari ya viwandani yakwama Bandarini Dar es Salaam

    (GMT+08:00) 2017-11-24 19:22:35
    Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) limesema sukari ya viwandani ya wanachama wake imekwama katika Bandari ya Dar es Salaam kwa wiki mbili sasa, jambo linaloweza kuathiri uzalishaji.

    CTI imesema wanashindwa kuiondoa sukari hiyo baada ya kukosa kibali cha kufanya hivyo kutoka Bodi ya Sukari kwa kile kinachoelezwa kuwa ni agizo la Serikali kuzuia uagizaji wa bidhaa hiyo.

    Hata hivyo, mtaalamu wa sera wa CTI, Akida Mnyenyelwa alisema agizo hilo halikulenga sukari hiyo inayotumika viwandani kuzalisha bidhaa za aina tofauti kama vile dawa na vinywaji baridi.

    Alisema kutokana na zuio hilo, baadhi ya viwanda vimekosa sukari kwa ajili ya uzalishaji wa bidhaa licha ya taratibu zote muhimu za kuingiza mzigo huo kufuatwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako