• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Benki ya maendeleo Afrika kujenga barabara ya Tabora - Mpanda

    (GMT+08:00) 2017-11-27 18:17:51
    Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) imeipa zabuni Kampuni ya China kujenga barabara ya kutoka Tabora hadi Mpanda kwa kiwango cha lami.

    Kampuni hiyo, M/s Jiangxi Geo-Engineering (Group) Corporation kutoka jijini Jiangxi, inatarajiwa kutumia miezi 36 kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 108 pamoja na miundombinu mingine.

    Kwa mujibu wa taarifa ya AfDB kuhusu zabuni hiyo iliyoombwa na washiriki sita wengi wakitoka China, mradi huo utatumia Sh158.8 bilioni.

    Miundombinu mingine itakayoambatana na barabara hiyo ni mitaro ya maji, madaraja na njia za mchepuko.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako