• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wanamichezo watano Urusi wafungiwa

    (GMT+08:00) 2017-11-28 12:44:51
    Kamati ya kimataifa ya Olimpiki IOC imewafungia, kutoshiriki tena mashindano ya Olimpiki, wanamichezo watano wengine wa Urusi kufuatia uchunguzi dhidi ya matumizi ya dawa za kuongeza nguvu michezoni zilizoharamishwa.

    Waliofikwa na adhabu hiyo ni Aleksei Negodailo na Olga Vilukhina ambao ni washiriki katika michezo ya kuteleza kwenye barafu, na wengine Sergei Chiduniov, Dmitry Trunenkov na Yana Romanova ambao ni mahodari katika michezo ya kulenga shabaha.

    Mpaka sasa IOC imewafungia wanamichezo 21 kutoka Urusi na imeendelea kuchukua maamuzi hayo kufuatia ripoti ya mamlaka ya kupambana na matumizi ya dawa za kuongeza nguvu michezoni WADA kuhusu Urusi.

    Kamati hiyo pia inatarajiwa kutolea maamuzi ya eidha timu za urusi kushiriki au kutoshiriki katika Olimpiki ya majira ya baridi nchini Korea Kusini mwaka 2018.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako