Licha ya kutajwa kuwa na uzoefu mdogo, Gattuso ameendelea kutazamwa kama tumaini jipya la klabu yake hiyo ambayo mpaka sasa imeonekana kutofanya vizuri kwa misimu minne mfululizo, ambapo ilishindwa kumaliza katika nafasi tano za juu kwenye msimamo wa ligi.
Timu alizowahi kufundisha Gattuso ni Sion akiwa kocha mchezaji, Palermo, OFI Crete, na mpaka anateuliwa kuiongoza Milan alikuwa kocha mkuu wa timu ya vijana ya AC Milan.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |