Mkutano wa ngazi ya juu wa mazungumzo kati ya Chama cha Kikomunisti cha China na vyama vya siasa duniani umemalizika leo hapa Beijing.
Mkutano huo umepitisha Pendekezo la Beijing na kusisitiza kuwa vyama vya siasa vinapaswa kuzidisha hali ya kuaminiana, kuongeza mawasiliano na uratibu kati yao na kutafuta kujenga uhusiano wa aina mpya wa vyama wa kutafuta mambo sawa na kuweka kando tofauti, kuelewana na kufundishana katika msingi wa uhusiano wa aina mpya wa kimataifa, na kuchangia nguvu zaidi katika kujenga jumuiya ya binadamu yenye hatma ya pamoja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |