Mkutano wa kwanza wa Baraza la haki za binadamu kati ya nchi za Kusini-Kusini umefunguliwa leo mjini Beijing. Rais Xi Jinping wa China ametoa barua ya pongezi ya kufunguliwa kwa mkutano huo, akisisitiza kuwa mambo ya haki za binadamu duniani hayatapata maendeleo bila ya juhudi za pamoja za nchi zinazoendelea duniani. Pia amesema anatumai kuwa jumuiya ya kimataifa itafuata moyo wa haki, usawa, kufungua mlango na kuwa na uvumilivu, kuheshimu na kuonesha matakwa ya watu wa nchi zinazoendelea duniani, kuhimiza watu wa nchi hizo kuwa na haki za kutosha za binadamu, ili kutimiza maendeleo ya pamoja ya binadamu wote duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |