Kahawa ya Uganda aina ya Robusta imeanza kuvutia soko la China.
Akizuguzma za vyombo vya habari nchini humo baada ya kurejea kutoka kwa maonyesho ya kahawa ya kimataifa ya Hainan nchini China, mkurungezi wa chama cha wakulima wa kahawa Joseph Nkandu, alisema soko la China ni fursa kubwa na litasaidia Uganda kuuza kilo milioni 20 za Robusta ifikapo mwaka 2010.
Alisema kahawa aina hiyo ilikuwa na bei ya juu ya dola 60 kwa kilo ambayo ni mara dufu ya aina ya Arabica.
Tayari serikali ya Uganda kupitia kwa mamlaka ya kahawa nchini humo inafanya kampeni za kuongeza mauzo nchini China na imefungua maduka kadhaa.
Uganda huzalisha na kuuza nje asilimia 85 ya kahawa aina ya Robusta.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |